Ilikuwa mapema Jumamosi ya wiki hii kwenye mji mdogo wa Magugu Babati
Vijijini ambapo wafugaji, wakulima, wafanyabiashara/wajasiriamali na
wananchj kutoka vijiji mbalimbali vya Mkoa wa Manyara, mikoa/wilaya
karibu kama Arusha, Kondoa n.k walikutanika kwenye mnada kijijini hapo
kwa madhumuni ya kuuza na kununua mifugo, mazao na bidhaa mbalimbali.
Mnada ulikuwa umechangamka, bidhaa za kutosha na idadi kubwa ya watu.
Angalia kwenye picha.....
 |
| Sagulasagula ya nguo ikiendelea, wateja wakijinunulia nguo kwa bei poa kabisa |
 |
| Kama ilivyokuwa kawaida kwenye minada/magulio ya aina hii kitu cha
nyama choma hua akikosekani, pichani mdau mmoja kama alivyobambwa na
camera yetu akingojea nyama ziive. |
 |
| Wadau hawa walikutwa na canera yetu wakitafuna nyama choma kwenye moja
la banda la mamalishe ama mama pima kama wanavyojulikana kwenye baadhi
ya maeneo |