Sunday, September 22, 2013

KAMERA YETU WEEK END HII IMEANGAZA MNADANI MAGUGU

 Ilikuwa mapema Jumamosi ya wiki hii kwenye mji mdogo wa  Magugu Babati Vijijini ambapo wafugaji, wakulima, wafanyabiashara/wajasiriamali na wananchj kutoka vijiji mbalimbali vya Mkoa wa Manyara, mikoa/wilaya karibu kama Arusha, Kondoa n.k walikutanika kwenye mnada  kijijini hapo kwa madhumuni ya kuuza na kununua mifugo, mazao na bidhaa mbalimbali. Mnada ulikuwa umechangamka, bidhaa za kutosha na idadi kubwa ya watu.
 Angalia kwenye picha.....
Sagulasagula ya nguo ikiendelea, wateja wakijinunulia  nguo kwa bei poa kabisa

Kama ilivyokuwa kawaida kwenye minada/magulio ya aina hii  kitu cha nyama choma hua akikosekani, pichani mdau mmoja kama alivyobambwa na camera yetu akingojea nyama ziive.


Wadau hawa walikutwa na canera yetu wakitafuna nyama choma kwenye moja la banda la mamalishe ama mama pima kama wanavyojulikana kwenye baadhi ya  maeneo

No comments:

Post a Comment