Saturday, August 24, 2013

Picha za mbio za mwenge mkoani Dodoma

Viongozi wa Mkoa wa Dodoma na Wakimbiza Mwenge kitaifa 2013 kwa pamoja wakiwasalimu viongozi/Timu ya Mkoa wa Morogoro (haipo pichani) iliyokuja kupokea mwenge kutoka Mkoa wa Dodoma.
Makamanda wakiulinda Mwenge wa Uhuru wakati wa kuukabidhi Mkoa wa Morogoro mara baada ya kumaliza mbio zake kwenye Mkoa wa Dodoma.
Vijana wa Kikundi cha hamasa kutoka Dodoma wakishangilia wakati wa makabidhiano ya Mwenge wa Uhuru baina ya Mkoa wa Dodoma na Morogoro yaliyofanyika kwenye kijiji cha ukwamani majawanga Kongwa kilichopo mpakani mwa Mikoa hiyo miwili.
Mkuu wa  Mkoa wa Dodoma Dr. Rehema Nchimbi (kulia) akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Joel Bendera wakati wa sherehe za makabidhiano ya Mwenge wa Uhuru kwenye kijiji cha ukwamani majawanga Kongwa kilichopo mpakani mwa Mikoa ya Dodoma na Morogoro.
Mkuu wa  Mkoa wa Dodoma Dr. Rehema Nchimbi (kulia) akimkabidhi Mwenge wa Uhuru Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Joel Bendera kwa ajili ya kuukimbiza Mkoani humo.

No comments:

Post a Comment