![]() |
| .Baadhi ya makaburi wa wapigania uhuru wa Nchi za Msumbiji, Afrika Kusini na Zimbabwe yaliyo katika Wilaya ya Kongwa. |
WILAYA ya Kongwa ilianza kujulikana katika ramani ya dunia
mwaka 1913 kutokana na Shirika la kidini kutoka Canada lililojulikana kama
Church Missionary Society (CMS) kujenga Chuo cha Ualimu na Theolojia katika
Kijiji cha Mlanga mwaka 1909.
Pia Kongwa ilipata umaarufu baada ya vita kuu ya pili ya dunia
ambapo Shirika moja la kilimo la Uingereza lililojulikana kama Overseas Food
Cooperation kuanzisha utafiti wa kilimo cha karanga .
Hata hivyo mwaka 1949 wilaya hiyo ilifutwa kutokana na
kushindwa kwa mradi wa karanga hali iliyosababishwa na ukosefu wa mvua kwa
miaka mitatu mfululizo jambo lililolazimu Shirika la Oveseas kufunga shughuli
zake.
Kabla ya Uhuru Wilaya ya Kongwa ilikuwa ikiongozwa na Watemi
au Machifu wa makabila ambao ndio walikuwa wanatawala maeneo mbalimbali kwa
kurithishana.
Mtemi Nuyanji alitawala eneo la Pandambili, Mtemi Mahinyika
akitawala Kongwa, Mtemi Kasawa alitawala Mlali na mtemi Simango alitawala eneo
la Sagara.
Hata hivyo baada ya Tanzania kupata uhuru, mfumo machifu
ulibadilika na kuwa mfumo wa
kidemokrasia ambapo jamii husika ilikuwa ikichagua kiongozi waliyemtaka.
Wakazi wa Kongwa ni Wagogo, Wakagulu, Warangi na makabila
mengine ambayo yalihamia kutoka sehemu mbalimbali za Tanzania kama Wabena,
Wanguu, Wangoni, Wakamba na Wamasai ambao walifika hapo kwa ajili ya shughuli za kilimo na ufugaji.
Kwa Mujibu wa Mkuu
Wilaya ya Kongwa, Alfred Msovella,Wilaya ya Kongwa ilianza mwaka 1996
chini ya sheria ya Serikali za mitaa ya mwaka 1982.
Wilaya hiyo ina ukubwa wa eneo la kilomita 4,041 ambapo eneo
linalofaa kwa kilimo na ufugaji ni hekta 363,690 ambapo wilaya ina tarafa tatu
za Kongwa, Mlali na Nzoisa, kata 22, vijiji 87, miji midogo miwili ya Kongwa na
Kibaigwa.
![]() |
| Mwandishi wa makala haya akitoka ndani ya handaki lililotumiwa na wapigania uhuru wa Msumbiji. |
Kwa mujibu wa sense ya watu na makazi ya mwaka 2012 na kwa
kuzingatia ongezeko la watu la asilimia 2.4 katika mwaka 2014 wilaya hiyo
inakadiriwa kuwa na jumla ya wakazi 324,296
Unapofika katika kambi ya wapigania uhuru iliyopo katika
Wilaya ya Kongwa Mkoani Dodoma utaona ni jinsi gani Baba wa Taifa hayati Mwalimu
Julius Nyerere alivyojitoa na kutoa ardhi ya Tanzania ili itumike kama njia ya
ukombozi kwa Nchi nyingine za Afrika.
Unapozungumza na watu mbalimbali wanaeleza jinsi baba wa T aifa
alivyoamua ardhi ya Kongwa na Tanzania kwa ujumla itumike kwa ajili ya mafunzo
ya kijeshi ili nchi zipate uhuru na kuutokomeza ukoloni na ubaguzi wa rangi.
Nafika kwenye kambi hiyo, najionea nyumba ambayo aliwahi
kuishi Rais wa kwanza wa Msumbiji Samora Machel na hata nyumba aliyowahi kuishi
Rais wa kwanza wa Namibia Sam Nujoma.
Japo baadhi ya majengo ya kambi hiyo yamekuwa yakitumika kama
shule, majengo mengine yanaonekana kuanza kubomoka na kutishia kupotea kwa
historia hiyo ambayo inaweza kutumika kama njia ya kujifunza japo kuna watafiti
kutoka mataifa mbalimbali wamekuwa wakitebelea kambi hiyo kujifunza.
Mwenyekiti wa halmashauri ya Kongwa, White Zuberi anasema,
alisema wilaya hiyo ina historia pana kutokana na kuwa na kambi ya ukombozi ya
wapigania uhuru wa Afrika.
Kwa Mujibu wa Mwenyekiti huyo wa halmashauri kambi hiyo
ilijengwa mwaka 1964 ambapo wapigania uhuru kutoka nchi za Msumbiji, Angola,
Zimbabwe, Namibia na Afrika kusini walikuwa wkiishi kawenyr kambi hiyo.
Pia kuna nyumba ambazo walikuwa wakiishi Samora Mashel abaye
alikuwa Rais wa kwanza wa Msumbuji na sam Nujuma Rais wa Namibia.
Zuberi anasema wliomfahamu Sam Nujoma wakati huo, walisema
alifiia hatua ya kuongea hata kidogo.
“Alipokuwa akipita kijijini walikuwa wakimsalimia Mlimswano-
kwa maana ya habari gani kwa kigogo lakini Nujoma alikuwa akidhani walikuwa
wakimuuliza habari za Chama cha ukombozi cha Namibia Swapo ambalo kinaelekea
kufanana na salamu hiyo” anasema
Lakini alipofahamu kama hiyo ni salamu akawa akiitikia kam
salamu lakini alijua kiasi lugha ya kigogo kutokana na kukaa na watu wa Kongwa
kama ndugu.
Baada ya kambi hiyo kufungwa kutokana mwa wapigania uhuru hao
kuondoka miaka ya 1980 majengo hayo yakachukuliwa na Jeshi na yalitumika mpaka
mwaka 1995 yakaanza kutumika kama shule
ya sekondari ya Kongwa.
Pia Mkuu wa majeshi wa sasa Davis Mwamnyange aliwahi kuwa mkuu
wa kambi hiyo ambayo wakati huo ilikuwa Kambi ya Maafisa Usalama wa Jeshi.
Aidha kuna makaburi ya wapigania uhuru hao ambao walifariki
wakati wakiwa kwenye kambi hiyo na waliozikwa na wanajeshi kutoka Namibia,
Afrika kusini na Msumbiji.
“Hata viongozi wa nchi hizo na ndugu wa marehemu hufika
kutembelea makaburi hayo na kuyasafisha, huwa tunapokea wageni wengi tu kila
mwaka” anasema
Hata hivyo anasema sasa wanafanya mazunguzo na serkali ili
eneo hilo liwe la makubusho ya kihistoria na hata kushawishi Jeshi la Ulinzi
waone huo ni urithi mkubwa kwa nchi na wanatakiwa kuutunza na kuuenzi.
Pia anakumbuka mwaka 2000, Meja Jenerali Romano kutoka Afrika
Kusini alifika hapo kutembelea kambi hiyo akiwa na kikosi cha Afrika Kusini na
hata Septemba mwaka huu alifika Waziri aliyekuwa akishughulika na wapigania
uhuru wa vita vya ukombozi.
“Bado tunashawishi watu mbalimbali hasa zilizoshiriki kwenye
ukombozi wa nchi zao kutafuta namna ya kufanya ili kambi hiyo iwe na maana pana
ana kuliko hivi sasa.
“Kuna historia pana sana hapa kuna madarasa na mabweni ambayo
yalitumiwa na watu ambao baadaye walikuja kuwa marais tunaona kuja tu hapa
haitoshi tunataka kitu kifanyike ili Kongwa ijivunie utajiri huu siku moja”
anasema
![]() |
| Madarasa yaliyotumiwa na wapigania uhuru. |
Kwa mujibu wa Mwenyekiti huyo wa halmashauri, katika historia
ya baba wa taifa kama kuna jambo kubwa ambalo alifanya ni pamoja na kutoa kambi
na ardhi itumike na nchi nyingine.
“Kambi hii iliasisiwa na Umoja wa Nchi za Afrika (OAU) na hilo
likaruhusu wapigania uhuru wan chi nyingine kufika Kongwa kuchukua mafunzo ya
kijeshi” anasema
Anasema Rais Jakaya Kikwete ametoa ahadi ya kujenga mnara wa
kumbukumbu ambao utachukua historia za nchi zote sita za Afrika ambazo zilifika
Kongwa kutafuta ukombozi wan chi zao.
Pia anataka serikali kujenga vyuo katika Wilaya hiyo ili wau
wafike kujifunza na Mji huo kukua kutokana na kuwa na historia pama ya ujombozi
wa Afrika.
Historia inaonesha kuna Waingereza baada ya vita walifungua
shamba la karanga Kongwa lakini kutokana na kutofanya vizuri wakaamua kuanzisha
shamba la mifugo ambapo sasa ni kampuni ya Ranchi ya taifa (NARCO).
Afisa Mtendaji wa kongwa Mjini, Paul Mtutui anasema kambi ya
wapigania uhuru ya Kongwa aimekuwa na hostoria pana na vita ya ukombozi
kutokana na nchi mbalimbali kutafuta ukombozi wan chi yao wakiwa Tanzania.
Anasema licha ya kuwa na majengo yaliyotumika kwa ajili ya
wapigania uhuru hao pia kuna handaki ambalo lilitumiwa na wapigania uhuru wa
Msumbuji na chama cha cha Frelimo wakiongoza na samora Machel ambaye baadaye
alikuja kuwa Rais wa kwanza wan chi hiyo ilipopata uhuru mwaka 1975.
Anasema handaki hilo lilikuwa likitumiwa kwa ajili ya
kujificha na kufundishia wapigania uhuru.
Hata baada ya wanajeshi hao kuondoka kambi ya Jeshi ilikuwa ikitumia majengo hayo.
Pia Klabu ya pombe iliyokuwa ikitumia na wapigania uhuru hao
sasa imebadilishwa na kuwa kituo cha afya.
“Hata Rais wa Uganda, Milton Obote alipopinduliwa na Idd Amini
alikuja kujificha Kongwa” anasema
Anasema wakati huo Obote alikuwa amejificha kwenye safu ya
milima ya kiboriani eneo la Mlanga ambalo ni sehemu ya kata ya Kongwa.
“Hapa kuna makazi ya zamani ya
Samora Machel na kambi hii ilipofungwa wakahamia Mazimbu Morogoro lakini
hakukaa sana tangu atoke hapa nchi yake ikapata uhuru 1975” anasema
Pamoja na hayo anasema licha ya wapigania uhuru hao kuishi
hapo lakini waliacha watoto kwa wenyeji.
“Walikuwa wakifika kijijini, wakawa na mahusiano na watu wa
huku, walipoondoka waliacha watoto wengi tu na sasa kuna watoto wengi wa askari
wa Namibia” anasema
Japo ni miaka mingi ilimepita lakini kuna watoto waliachwa na
wanajeshi hao japo wengine walichukuliwa na baba zao wakati wakindoka Tanzania.
Anasema mwaka 1996 alifika Askari wa Namibia ambaye alishiriki
kwenye kambi ya wapigania uhuru, Nakonkwa,
akakusanya watoto ambao baba zao ni wanajeshi wa Namibia na akaahidi
kuwafuata watoto waliobaki lakini mpaka saa hajaonekana tena kurudi.
Anasema watoto waliochukuliwa wakati ule walikuwa sita wenye
umri wa miaka kati ya 15 na 17.
“Wengine bado hapa kijijini mpaka sasa na wengine wana wajukuu
wameshakuwa watu wazima sasa” anasema
Anasema mmoja wa watoto wa wanajeshi hao ambaye ni msichana
aliyechukuliwa wakati wapigania uhuru hao kuondoka, ameamua kurudi Kongwa
kutoka Namibia.
Kaimu Afisa Maenseleo ya Jamii Wilaya ya Kongwa, Pascalina
Duwe anasema huo ni urithi mkubwa katika vizazi vya sasa na vijavyo na kuna
kila sababu kwa watanzania kutembelea kambi hiyo ili kujifunza namna Tanzania
ilivyoshiriki kwenye vita vya ukombozi wa nchi nyingine.
Mkuu wa Wilaya ya Kongwa, Alfred Msovella anasema, historia ya
Mji huo ni pana ikihusishwa na uwepo wa ukoloni na uchumi wa kikoloni ambao
unajionesha kupitia mradi wa karanga ambapo baada ya mradi huo kushindwa
wakoloni wakawa na wazo la kuanzisha ranchi mwaka 1948 baada ya vita ya pili ya
dunia.
Anasema hapo kukawa na ujenzi wa reli na sura ya kuuza mazao
na uwepo uchumi wa kikoloni.
Anasema historia ya ukombozi kusini mwa Afrika ilifanya
mataifa ya Afrika yapate uhuru wake kwa kutumia miundombinu waliyoaha
wakoloni kuwa mahali pa kufundishia wapigania uhuru na hata Marais Samora
Machel na Sam Nujoma.
“Kwa kutumia miundombinu iliyoachwa na wakoloni wakaona
watumie kuweka kambi ya wapigania uhuru jambo zuri hata Marais kama Samora na
Nujoma waliwahi kuishi Kongwa” anasema
Hata nyumba aliyokaa Samora ilifanana na zile za Shirika la Reli
kwani inavyoonekana ni mengo ambao
shirika la reli limekuwa likitumia katika ujebzi wa nyumba zake1980
zimambwe, 1990 namibia
Mkuu huyo wa Wilaya anasema baada ya Nchi zote kupata uhuru
likafuata suala la kukomesha ubaguzi wa rangi hasa nchi Afrika Kusini.
Pia anasema utajiri mwingine wa kihistoria uliopo kongwa
ulikuwa ni uenezaji wa dini hasa Anglikana kulichochewa na kuwepo kwa Chuo cha
Theolojia cha Mlanga ambapo maaskofu wengi wa zamani walipata mafunzo hapo na
viongozi wengi wa kanisa wamepitia hapo.
Anasemma ukitazaa matukio yote hayo, Chuo cha Interejensia,,
mahandaki, sehemu aliyoishi Samora na Sam Nujoma na ukombozi wenyewe ni fursa
muhimu utalii wa kiutamaduni unaoweza
kufanyika katika eneo hilo.
Anasea hata ukifika Narco Konga kuna behewa kubwa la treni
ambalo lina historia ya wakoloni ni fursa nzuri ya watu kutembelea kujifunza.
Pia hata watu waliopita Mlanga wana historia kubwa ya
kujifunza, kuna shule za wakoloni, hospitali ya kuaminika vyote ni fursa nzuri
za kutembelea na kujifunza.
“Waziri aliyepigania vita vya uhuru wa Afrika Kusini alikuja
hapa na wenzetu huko kwao fursa hii zinatumika kama sehemu ya utalii kama
chumba alicholala Nelson Mandelea alipokuwa gerezani sasa ni utalii mzuri sana
watu wanatembelea na sisi tunatakiwa kufanya hayo” anasema
Pia anasema Samora aliishi sana Kongwa na kuna aminika kuwa
kwenye handaki kulikuwa na njia ambayo ilikuwa ikipita chini kwa chini hadi
kwenye nyumba aliyokuwa akiishi.
“Kitendo cha kufanya eneo lile kuwa shule kutafuta ile
historia iliyopo tungefanikiwa kila kitu kilichopo kungekuwa na sehemu kubwa ya
utalii kwani hata watu waliokaa pale wana ushuhuda mkubwa zaidi” anasema
Msovella anasema kuna wazungu waliishi Kongwa miaka ya nyuma
lakini walipofika Kongwa wameshangaa kwa
nini Kongwa inakuwa kame.
Anasema miaka ya nyuma Kongwa ilikuwa na maji mengi lakini
sasa imekuwa kame kutokana na uharibifu wa mazingira.







