Huku akinukuu ripoti ya Benki ya Dunia ya Programu ya Usafi wa Maji na Mazingira iitwayo ‘Madhara ya Kiuchumi yatokanayo na hali duni ya usafi wa mazingira afrika’, Bw. Kema alisema kuwa fedha hizi ni nyingi na kwamba zingeweza kuokolewa kama usafi wa mazingira ungeboreshwa nchini.
Kwa mujbu wa ripoti hiyo, jumla ya Watanzania milioni 26 wanatumia vyoo duni na pia zaidi ya watu milioni tano hawana choo na kwamba wanajisadia haja ndogo na kubwa kwenye maeneo ya wazi.
Pia inaonesha kuwa mtu mmoja asiye na choo bora hupoteza muda wa siku mbili na nusu kwa mwaka katika kutaafuta eneo la kujisadia katika maeneo ya wazi ili watu wengine wasimuone.
Mafunzo hayo yaliyoandaliwa na mradi wa UMATA yalifunguliwa rasmi na Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Betty Mkwasa.
Kwa mujibu wa Mkwasa alisema pamoja na kwamba Dodoma ina matatizo makubwa ya upatikanaji wa maji lakini hilo lisiwe kisingizio cha kutotiliaa maanani usafi wa mazingira.
“Hatuwezi kuacha wananchi wasijali usafi kkwa vile
kuna tatizo la maji , usafi wa mazingira si kuoga tu ni usafi wa jumla katika
kaya na hata kuhakikisha kuna choo bora” alisema
Mradi huo unafadhiliwa na mfuko wa Umoja wa Mataifa
wa Usafi wa Mazingira (GSF) na kutekelezwa na Shirika la Plan International
katika wilaya za Bahi, Chamwino na Kongwa mkoani Dodoma.


No comments:
Post a Comment