Friday, December 5, 2014

Mkazi wa mpwapwa ajifungua mtu kama chura

MKAZI wa  wa   kijiji cha  Chibwechangula –Behelo  katika Wilaya ya
Mpwapwa Mkoani Dodoma, Ruth Matonya (26)  amejifungua mtoto wa ajabu
ambaye nusu ya sura yake ilikuwa ikifanana na binadamu na nusu
ikifanana na chura.
Mtoto huyo alizaliwa Desemba 2, mwaka huu katika Kituo cha Afya cha
Mtakatifu Luka  kinachomilikiwa na Kanisa la Anglikana  Dayosisi ya
Mpwapwa. Ambapo alifariki dakika chache baada ya kuzaliwa.
Kwa mujibu wa Mganga Mfawidhi wa kituo hicho Dk. Edwin Kihura  mara
baada ya mama huyo kufika kituo hicho cha afya alikuwa na uchungu
mkali  ambao uliendelea bila kukoma na baadaye alishindwa kujifungua
kwa njia ya kawaida licha ya kuwa njia ilikuwa imefunguka.
Alisema kutokana na hali hiyo ilimazimika mama huyo kufanyiwa upasuaji
 ili kuweza kuokoa maisha yake na mtoto.
Alisema  wakati mama huyo akihudhuria kliniki walipojaribu kupima
miezi ya mwisho mama huyo  lakini mkao wa mtoto ulikuwa haupatikani,
wala mapigo  ya mtoyo yalikuwa hayapatikani lakini mtoto alikuwa
anacheza tumboni jambo ambalo lilikuwa likiwashangaza sana  waganga na
manesi kituoni hapo.
Dk. Kihura alisema mara baada ya mama huyo kufanyiwa upasuaji
waliweza kutoa mtoto wa jinsi ya kike  ambae alikuwa na  sura isiyo
eleweka na kichwa kilikuwa nusu  na sura ya binadamu na nusu ikiwa ni
sura inayofanana na chura lakini viungo vyake vyote vikiwa kamili.
Alisema zipo sababu kadha ambazo  zinazoweza kusasabisha tatizo kama
hili ambapo alisema kuwa ni  baadhi ya akina mama kukosa baadhi ya
madini mwilini na  uumbaji kuto kamilika ambao unasababishwa na sababu
za kibailojia   ambazo ni kushidwa kugawanyika kwakromozome.
Alisema tatizo hilo kitaalam linajulikana kama Anecephaly.
Pia alisema matatizo kama hayo huweza kutokea  mala chache sana katika
hospitali nyingi lakini vitendo hivi vimekuwa vikiongezeka  kwa wingi
kwa siku za hivi karibuni .
Alisema hali ya mama huyo inaendelea vizuri  na pia huyo alikuwa ni
mtoto wake wa tano.

No comments:

Post a Comment