Monday, March 2, 2015

Walimuoza binti mdogo kusota rumande mpaka kesi iishe



MKE na Mume wanaotuhumiwa kumuoza binti wa miaka 10 jana walifikishwa
katika mahakama ya Wilaya ya Dodoma Mjini huku mahakama ikifunga
dhamana yao hadi kesi hiyo itakapomalizika.
Washtakiwa hao wanakabiliwa na shtaka la kumuozesha mtoto mwenye umri
wa miaka 10 ambaye ni binti yao.
Mbele ya hakimu mkazi wa mahakama ya Wilaya Dodoma Mjini , Mwajuma
Lukindo Mwendisha mashitaka wa Serikali Lina Magoma alidai washtakiwa
Stephano
Nyambuya (65) na mkewe Juliana Gidion (30) ambao ni wakazi wa kijiji cha Lionii
wilayani Bahi mkoani Dodoma walitenda kosa la kumuozesha mtoto aliye
chini ya miaka 15
Mwendesha mashitaka huyo alisema watuhumiwa hao walitenda kosa hilo
kinyume cha  kifungu cha sheria namba 138  (2) cha kanuni ya adhabu
kilichofanyiwa marejeo mwaka 2002.
Magoma alisema wazazi na walezi hao waliamua kumuozesha mtoto aliye
chini ya umri huo kwa Joshua Mnamba mwenye umri wa miaka (25), ambapo
wote kwa pamoja walikana shitaka lao.
Hakimu  mkazi Lukindo alisema washitakiwa hao
wanatakiwa kuwa rumande kutokana na kusa walilotenda kutokuwa na dhamana
Alisema kifungu cha sheria namba 148 (5) a (i) kinachozuia dhamana kwa
watu wenye makosa kama hayo, hivyo washitawa watabaki
rumande mpaka kesi yao itakapokwisha.
Kesi hiyo itatajwa tena Machi 16, mwaka huu
Mnamba ambaye alimuoa binti huyo alifikishwa mahakamani hapo Februari
24, mwaka huu na yuko rumande.
Mshtakiwa huyo alishtakiwa kwa kosa la kubaka.
Kwa sasa motto huyo aliyeozwa amepata hifadhi kwa mkuu wa Wilaya ya
Dodoma Mjini Betty Mkwasa.
Kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo kulifuatiwa taarifa zilizotolewa na
majirani kwa serikali ya kijiji na hatimaye Polisi na watuhumiwa
kufanikiwa kukamatwa.
Mtotohuyo alikuwa ameozwa kwa mahari ya Sh. 100,000 na mbuzi 12.

No comments:

Post a Comment