Tuesday, April 22, 2014
Mila ya kuondoa mikosi 'kitigo' ilivyomsababishia Ukimwi
“NILIPATA maambukizi ya Ukimwi mwaka 1990, nakumbuka baada ya kifo cha mume wangu niliambiwa nirithiwe na mdogo wa mume jambo hilo nililipinga , nduguze wakasema kama sitaki kuolewa lazima uondoe kitigo (mkosi) bila hivyo utaua ukoo mzima huo ukawa ni mwanzo wa safari ndefu katika maisha yangu kwani baada ya muda mfupi nilianza
Nilimfahamu mwanamke huyu wakati wa kongamano la wanawake Kitaifa
“Mimi niko tayari wakati wowote na niko tayari kueleza kitu gani
Akiwa ni mwanaharakati wa masuala ya Ukimwi na hata nyanja za ukatili
Anasema kuwa,mume wake alifariki mwaka 1990 na wakati huo tayari
Hata hivyo,anasema kuwa,baada ya msiba huo kuisha wana ukoo walikaa na
Anasema kuwa aliambiwa hayo kabla hata hajamaliza eda, japo alikuwa
Ndipo ulipofika usiku akasindikizwa na mwanamke moja ambaye hamfahamu
Rukia anasema kuwa, baada ya miezi sita akaona afya yake inashuka na
Baada ya kupima akagundulika kuwa ana maambukizi ya Virusi vya Ukimwi
Hata hivyo alipewa rufaa ya kwenda hospitali ya Bombo kwa ajili ya
‘Nilipewa mlolongowa chakula ambachokitanisaidia na mambo ambayo
Anasema kuwa mwanaume aliyemfanyia kitigo ndiye atakuwa amemuambukiza
Japokuwa aliamua kumuachia Mungu juu ya maisha yake na kuamua kuishia
Hata hivyo anasema kuwa, mwaka 2006 alifiwa na binti yake aliyemtaja
Anasema kuwa tangu wakati huo ameendelea kutumia ARV lakini mpaka sasa
Rukia anasema kuwa,ameamua kuwa kioo cha jamii na amekuwa akielimisha
“Mwaka 1999 nilijitangaza kuwa ninaishi na virusi vya Ukimwi hiyo ni
Anasema baada ya kujitangaza kuna watu walikuwa wakimnyooshea vidole
Anasema kuwa,wito wake mkubwa kwa jamii ni kuwa kuona Ukimwi kama
“Ukimwi ni kama mafua watu wote wanakufa na makaburi yanachimbwa kila
Rukia anasema kuwa wenye virusi vya Ukimwi wanakupa mapema kutokana na
Anasema kuwa, kwa sasa maisha yake yana amani zaidi kutokana na
Pia anasema kuwa amekuwa akifanya kazi ya kutoa ushauri nasaha katika
Rukia anasema kuwa sasa Mungu amemjalia maisha yake na amani na
Anasema kuwa maisha yake ni ya amani na anamshukuru mumewe huyo kwa
“Watu wengine wanasema Rukia ni muongo kaamua tu kula hela kwa
Rukia ambaye anazifahamu ABC hazi Z za mbinu za kuepukana na Ukimwi
Anasema kuwa jamii ina nafasi nzuri za kujikinga na maambukizi ya
“Nawaambia vijana vyote ving’aavyo si dhahabu vingineni vya kuchovya
Pia anazitaja hatua nne za maambukizi kuwa ni pamoja na kipindi cha
Anasema hatua ya pili unakwenda kupima lakini maambukizi hakuna wala
Hatua ya tatu ni utata mwambata huwa ni kipindi cha utatanishi unakuwa
Rukia anasema kuwa hatua ya nne ni kipindi tuli ukidharau kutumia
Anasema kuwa ukifikia katika hatua hiyo dawa ni maombi, faraja na
Friday, April 18, 2014
Polisi dodoma wajipanga kudhibiti uhalifu sikukuu ya Pasaka
JESHI la Polisi Mkoani
Dodoma, limesema limejipanga kuimarisha ulinzi
maeneo yote ya Mkoa wa
Dodoma katika kipindi chote cha sikukuu ya
pasaka.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa
Dodoma Kamishna Msaidizi wa Polisi (SACP),
David Misime alisema
katika kipindi cha pasaka Jeshi la polisi
limejipanga kuimarisha
ulinzi maeneo yote ya mkoa wa Dodoma na
watafanya doria za miguu,
pikipiki, magari na pia kutumia mbwa na
farasi.
Alisema kutokana na suala
la ulinzi na usalama ni la kila mtu na wadau
mbalimbali na
watashirikiana na vyombo vingine vya dola, manispaa
kampuni za ulinzi
binafsi, viongozi wa serikali za mitaa na vikundi
vya ulinzi shirikishi.
“Tunachoomba ni kila mtu
atambue ulinzi ni jukumu la kila moja na
unaanzia katika ngazi ya
familia tunaomba waendelee kushirikiana na
Jeshi la polisi kwa
kutupatia taarifa za wahalifu na uhalifu” alisema
Alitaka kila
mtu azingatie sheria za usalama barabarani ili kuzuia
ajali,kuepuka ulevi wa
kupindukia na sehemu za starehe wazingatie
sherehe.
Sunday, April 13, 2014
Ukatili wa kijinsia ulivyoharibu ndoto za Felista
UKATILI wa Kijinsia ni miongoni mwa mambo ambayo
yamekuwa yakiathiri maendeleo ya wanawake. Kumekuwa na juhudi mbalimbali
zinazofanywa na Serikali na Mashirika yasiyo ya Kiserikali na hata yale ya
kimataifa kuhakikisha vitendo hivyo vinakomeshwa katika jamii.
Takwimu zinaonesha kuwa, ukatili wa wanawake
majumbani umeendelea kuongezeka, kati ya wanawake watatu, wawili wamefanyiwa
vitendo vya ukatili.
Asilimia 39 ya wanawake wenye umri kati ya miaka 15
hadi 49 wamefanyiwa vitendo vya ukatili wa kimwili na asilimia 20 ya wanawake
wamewahi kufanyiwa ukatili wa kingono.
Pia takwimu zinaonesha kuwa asilimia 45 ya wanawake
wamefanyiwa ukatili wa kijinsia na takribani wasichana watatu kati ya 10
wametendewa angalau tendo moja la ukatili wa kijinsia kabla ya kufikisha iaka
18.
Felister John
(30),mkazi wa Ruamlimi Wilaya ya Musoma Mkoani Mara ni miongoni mwa
wanawake waliowahi kukutana na vitendo vya ukatili wa kijinsia. Mwanamke huyo
ambaye sasa ni maarufu kutokana na kazi yake ya kuuuza mboga mboga anasema
kuwa, aliolewa mwaka mwaka 2001 akiwa na umri wa miaka16 baada ya kumaliza
elimu ya msingi.
Nilikutana na Felister wakati wa Kongamano la
Kitaifa la wanawake lililoandaliwa na Muunganio wa asasi zinazoshughulikia
masuala na kijinsia lililomalizika hivi karibuni mkoani Dodoma.
Licha ya ucheshi wake lakini ni mwenye historia
ndefu katika maisha yake ambapo wakati mwingine unaweza kuona hailingani na
umri wake.
Kulingana na Felista siku chache baada ya kufunga
ndoa wakaenda kijijini kwa mumewe
Tarime kusalimia na kufikia kwa shemeji
yake ambaye ni kaka wa mume wake .
Cha ajabu shemeji yake akaanza kumtaka kimapenzi jambo ambalo hakukubaliana nalo na huo ukawa
mwanzo wa kufanyiwa visa na kuna siku aliwahi kumtamkia kuwa kuna kitu kibaya atamfanyia
kwani yeye ni muolewaji tu.
Baada ya muda akaanza kuugua kichomi, ndipo shemeji
yake aliposema kuwa anataka amtengenezee dawa lakini cha kushangaza dawa
ilikuwa ni pilipili iliyokuwa imesagwa.
“Shemeji
aliweka mkaa kwenye sufuria , moto ulikuwa mkali, nikakalishwa chini nikaambiwa
nipanue mguu wakaweka moto chini ya miguu na kisha nikafunikwa na shuka na blanketi wakaja watu wakashikilia zile nguo nilizofunikwa
ili hewa isiingie wala kutoka na akawekwa pilipili kwenye moto zile pilipili zilipokuwa
zikiungua harufu ilikuwa kali nikaanza kushindwa kupumua” anasema
Anasema kuwa, alipofunuliwa nguo alizokuwa
amefunikwa ambazo ni blanketi na shuka alikuwa hajiwezi kabisa na tayari
alikuwa amejisaidia haja ndogo na alikaa kitandani siku tatu bila kutoka nje.
Shemeji yake akamuambia hiyo dawa inatakiwa irudiwe
baada ya siku tatu,lakini alikataa kata kata.
“Kwa kweli sikukubali akaenda kunishtakiwa kwa mume
wangu kuwa nilikuwa nikikataa na mume wangu akaungana na kaka yake kuwa ni
lazima nitumie dawa ili nipone, niliamua kukimbia lakini mume wangu
alinikimbiza hadi kunikamata na kwa
kushirikiana walifanikiwa kunifunika na kuniwekea tena ile dawa nikaanza kulia
kuwa ninaungua mapaja wakasema acha niungue kwani walikuwa wakinitengeneza
dawa” anasema
Baada yakuachiwa kutoka kwenye nguo alizokuwa
amefunikwa mguu ulikuwa umeungua vibaya akawa na maumivu makali sana hali
iliyosababisha kupoteza fahamu.
Hata hivyo baada ya fahamu kumrudia aligundua
amejisaidia haja ndogo na kwa vile walikuwa wamembananisha mguu gamba la mguu
wa kulia likabaki mguu wa kushoto na kufanya pale palipobanduka kuwa na kidonda
kikubwa.
“Nikaugua mwezi mzima hakuna wa
kunipelekahospitali,siwezi kutembea wala kunyanyuka najisaidia humo humo
ndani ikafikia hatua mguu ukanuka
wakaniletea manyoya ya sungura na asali wakaniwekea kwenye mguu ulioungua
wakasema hakuna kuosha mguu” anasema
Felista anasema kuwa,baada ya wiki mbili mguu ukawa
umeoza anakumbukailikuwa ni Agosti 3, mwaka 2001 akawa mtu wa ndani tu manyoya
ya Sungura aliyowekewa yalikuwa palepale lakini nyama za miguu zikawa
zikidondoka chinikutokana na kuoza.
“Nikafikiria
nifanye nini nikapata wazo la kuandika barua ili ndugu zangu wapate taarifa,
lakini nilipokuwa naandika barua shemeji akanikuta akachukua barua ile na
kuichana nililia sana maana sikujua hatma yangu itakuwa nini” anasema
Hata hivyo akapata wazolingine la kumtuma kijana wa
jirani kwenda stendi amtafute ndugu yake aitwaye Mashaka ili aweze kuwapatia taarifa nyumbani na kwa bahati
nzuri aliweza kuwapatia taarifa wakamtuma bibi mzaa mama akafika
Anasema kuwa,bibi yake alipofika alikuta akiwa na
hali mbaya na wakati huo alikuwa na mimba ya miezi saba na baadaye ikaamuliwa
apelekwe kijijini kwa mumewe kule Matongo
na baada ya kufika huko kikao kilikaa na kukubaliana apelekwe hospitali ya
Bugando bili akakatwe mguu lakini hata hivyo kaka yake Wambura Mwikwabe ambaye
anaishi Musoma alikataa.
“Wakanipeleka Musoma kwa kaka yangu nikaanza
kuhudumiwa na hali yangu ikawa nzuri na siku ambayo uchungu uliponianza nikaenda
hospitali na mama mkwe wangu lakini cha kushangaza aliniambia siumwi bali
nilikuwa nimetamani vitanda vya hospitali jinsi vilivyokuwa vimetandikwa na
kama nina uchungu mbona sioneshi dalili” anasema
Felista anasema kuwa,alijifungua siku hiyo hiyo
yaani Oktoba 21, mwaka 2001 na kupata mtoto wa kike na mama yake mzazi alifika
na kumhudumia na baada ya kuruhusiwa
kutoka hospitali akarudishwa tena nyumbani kwa mumewe huku akiendelea kuishi
kwa manyanyaso ikafikia hatua anarudi nyumbani kwao na kisha kwa mumewe.
Anasema kuwa mtoto wake wa kike aliyejifungua kwa
bahati mbaya alifariki wakati akiwa na
umri wa miezi tisa na alipobeba mimba nyingine kuna siku mumewe alimpiga na
mimba hiyo kutoka.
Hata hivyo tayari ana watoto wengine watatu Anna
mwenye umri wa miaka tisa anayesoma shule ya Msingi Nyakato akifuatiwa na Ayub
na Zacharia ambao bado wako chekechea.
Felista anasema kuwa mwaka 2012 likazuka jambo
jipya.dada yake alikuwa amelazwa hospitali na hilo likamlazimu kuchukua watoto
wa dada yake na kuishi na pale nyumbani.
Jambo hilolikamkera mumewe ambaye aliwafukuza watoto
hao wakati akiwa hospitalini akimuangalia mgonjwa.
“Baada ya kurudi sikuwakuta watoto wa dada, nilipomuuliza
mume wangu aliniambia kuwa watoto wale wana baba na mama na hawahitaji nyumbani
pale,nilishangaa kwa vile pale nyumbani kulikuwa na mama mkwe na watoto watano
na ndugu wa mume wangu,nikamwambia kama wale umewafukuza basi na hao wa ndugu wako nao waondoke kwani mtoa
matumizi alikuwa ni mimi na siko tayari kutoa matumizi tena, ukawa ugomvi
mkubwa” anasema
Anasema kuwa ugomvi huo ukaingiliwa na ndugu wa
mumewe akiwemo wifi yake Sophia ambao walikaa kikao na kuamua kumfukuza
“Nilikataa kuondoka kwa vile nyumba ile nilikuwa
nimejenga mimi na kiwanja ambacho tumejenga nyumba nilinunua mwenyewe kwa
Shilingi 250,000 kutoka kwa Sophia “ anasema
Anasema kuwa, fedha za kiwanja alitoa na kumpa
mumewe ili akalipie kiwanja hicho ambapo hata aliporudi na kuuliza kama
kulikuwa na kuandikishiana kwa ajili ya ushahidi mumewe alimuambia kwa vile
walikuwa ndugu hakuna sababu ya kuandikishiana.
“Baada ya kununua kiwanja hicho tulijenga nyumba ya
matofali mabichi lakini ikabomoka na mvua na mara ya pili tukajenga ya tofali
za kuchoma vyumba viwili na sebule.” anasema
Felista anakumbuka Julai 21, mwaka jana, mumewe
alimpiga hadi kwenda kulazwa wodini kwa siku tatu na wakati akiwa hospitali
wifi yake alitafuta gari na kutoa vitu vyote vya ndani na fedha taslimu
Shilingi milioni 1.3 lakini hata hivyo majirani wakapinga vitu hivyo kuondoka.
“Nilipopata taarifa nikaenda nyumbani nikakuta
Toyota Hiace iko nje wanapakia vyombo na vitanda,nikapiga yowe nikalala chini
ili gari lisiondoke dereva alipotaka kuondoa gari nikamwambia uniue hapa hapa siondoki” anasema
Anasema kuwa alipata ujasiri wa kupiga simu kwenye Shirika
la ABC Foundation ili kupata masaada kwani wana kitengo cha kutetea haki za
wanawake na watoto na wao wakapiga simu polisi,mara polisi wakafika na kukuta
baadhi ya watu wakishikiliwa na wananchi.
Miongoni waliokuwa wakishikiliwa ni Sophia, mdogo wa
mume wangu aitwaye Paul pamoja na mama mkwe.
Hata hivyo mume wa Sophia
alifanikiwa kukimbia na alipoingia chumbani alikuta fedha alizokuwa
amehifadhi hazipo.
Polisi wakaamua vyombo hivyo vishushwe na watuhumiwa
walifikishwa kituo cha polisi na wakafunguliwa mashaka.
Lakini watuhumiwa walikuwa wakicheleweswa kufikishwa
mahakamani lakini Agosti 3, mwaka jana
walifikishwa mahakama ya mwanzo Kitaji,Musoma.
Anasema kuwa kabla ya kufikishwa mahakamani
watuhumiwa hao polisi walikuwa wakimzungusha na hapo aliamua kwenda kwa Mkuu wa
Upelelezi wa Wilaya kuomba msaada jambo lililowachukiza askari na kusema kuwa
alikuwa akiwachongea kwa bosi wao kwani walikuwa wamemuambia alete shahidi ili
kesi iende Mahakama ya Wilaya.
Tangu kesi imefunguliwa mashahidi wamekuwa
wakizungushwa kilawakienda kesi inaahirishwa,.
“Lakini naamini mahakama itatenda haki kwani nyumba
ile ni yangu na hata fedha walizochukua naomba Mungu warudishe kwani nilikuwa
nikidunduliza muda mrefu kutokana na biashara yangu ya kuuza mboga mboga”
anasema
Anasema kuwa
mumewe tangu ampige na kukimbilia Tarime kwa kaka yake Julai mwaka jana, mpaka
sasa bado hajarudi na amekuwa akilea watoto peke yake.
Felista anataka wanawake kuvunja ukimya pindi
wanapofanyiwa mambo ya ukatili kwani ukatili umekuwa wakati mwingine ukikatisha
uhai na hata kusababisha vilema vya maisha.
“Wanawake wasikae kimya wanapofanyiwa ukatili, wawe
wazi ili waweze kusaidiwa,mimi naona kama nilikosea kuolewa na mwanaume yule
kwani mara kadhaa nimenusurika kupoteza maisha kutokana na kipigo” anasema
Anasema kuwalicha ya kufanyiwa ukatili mara kadhaa
ikiwemo kuchomwa moto, kupigwa hadi mimba kutoka na hata kutaka kudhulimiwa
nyumba lakini ameendelea kufanya shughuli zake kama kawaida kutokana na kutokaa
kimya kwani matukio mengi ya ukatili aliyokuwa akifanyiwa amekuwa akitoataarifa
hali ambayo mara nyingi hata majirani wamekuwawakimtetea pindi wanapoona kuwa
haki haikutendeka.
![]() |
Mguu wa Felista unavyoonekana kwa sasa baada ya
kupona
|
![]() |
2.Felista akizungumza wakati wa kongamano la kitaifa
la wanawake lililofanyika Mjini Dodoma.
|
Safari bado ndefu kufikia usawa wa kijinsia
Na Mwandishi Wetu
“LAZIMA wanawake wajengewe uwezo tunataka nchi inayojali usawa wa kijinsia, hatutaki kusikia maneno ya kejeli kwa wanawake wanaojitokeza kugombea uongozi kwa lengo la kuwavunja moyo ili warudi nyuma”
Maneno hayo yanasemwa na mwanasiasa Mkongwe na Mbunge wa viti maalum Anna Abdallah wakati wa mkutano wa Umoja wa Wanawake Wanasiasa nchini (Ulingo) uliofanyika Mjini Dodoma.
Anabainisha kuna umuhimu kwa vyama vya siasa kuwa na demokrasia ya kweli kwani bila kufanya hivyo mfumo wake wa uendeshaji kamwe hauwezi kujali usawa wa kijinsia.
Kulingana na Abdallah vyama vingi vya siasa havina usawa wa kijinsia jambo ambalo linahitaji kufanyiwa kazi. Pamoja na hayo anasema ataendelea kukemea vitendo vya kudhalilisha wanawake wanaotafuta uongozi.
Abdallah ambaye ni Mwenyekiti wa Ulingo anasema ataendelea kuwa mkali kuona wanawake wanaotafuta uongozi
wanapodhalilishwa kwani wengi wao wamekuwa wakinyanyasika kwa kauli chafu na maneno ya kejeli kuwa hawawezi uongozi.
" Ndani ya siasa wanawake wananyanyasika hasa pale wanapotafuta uongozi, utasikia mtu anasema wewe utamchaguaje mwanamke ambaye
anachuchumaa wakati wa kwenda haja, haya si maneno mazuri mtu wa namna hiyo anamdharau mwanamke ambaye ni sawa na mama yake mzazi " anasema
Kulingana na mwanasiasa huyo wanataka kuweka wazi
kuwa mwanamke ana nafasi waheshimiwe kwani hata vijana wamekuwa na misemo ya
ovyo juu ya wanawake wakati wamezaliwa na wanawake hao hao ambao wanawakosea
adabu.
Anasema kuna haja ya kuwajengea uwezo wanawake
waonekane wana uwezosawa na wanaume na kuondoa misemo ya ovyo.
“Tunapopata nafasi lazima tuelezane na tujengeane
uwezo wanawake wana fursa, nia na uwezo
hasa pale wanapochaguliwa kuwa viongozi” anasema
Anabainisha kuwa bunge la sasa la katiba lina wajumbe zaidi ya 600 ambapo wajumbe 201 wanatoka maeneo mbalimbali na sasa kinachofanyika ni kuwajengea uwezo wanawake ili watakapokwenda kwenye kamati wapate
kuwasemea wanawake wenzao.
"Lazima tuelezane na kujengeana uwezo tunataka nchi inayotetea usawawa kijinsa lazima ifike wakati ionekane kila mtu ana thamani sawa" anasema
Anabainisha kuwa bunge la sasa la katiba lina wajumbe zaidi ya 600 ambapo wajumbe 201 wanatoka maeneo mbalimbali na sasa kinachofanyika ni kuwajengea uwezo wanawake ili watakapokwenda kwenye kamati wapate
kuwasemea wanawake wenzao.
"Lazima tuelezane na kujengeana uwezo tunataka nchi inayotetea usawawa kijinsa lazima ifike wakati ionekane kila mtu ana thamani sawa" anasema
Aidha maslahi ya wanawake wa Tanzania yanaendana na uwazi na hapendi kuona kunakuwa
na udhalilishaji ua utoaji wa maneno machafu kwa wanawake wanaojitokeza
kugombea nafasi mbalimbali
Mbunge wa Viti Maalum, Suzan Lyimo(Chadema) anataka wanawake walio bungeni kuwaunga mkono na kuwachagua wanawake wanaogombea nafasi mbalimbali .
Mbunge wa Viti Maalum, Suzan Lyimo(Chadema) anataka wanawake walio bungeni kuwaunga mkono na kuwachagua wanawake wanaogombea nafasi mbalimbali .
Pia katika rasimu ya kwanza amani ilikuwa ni moja ya
tunu ya taifa lakini katika rasimu ya pili tunu hiyo haipo na wana jukumu la kuhakikisha
tunu ya amani inarudi ili kwenda sambamba na mambo mengine.
Anataka Ulingo kusimama na kukemea hasa pale ambapo
wanaona mwanamke anadhalilishwa, hata anapofanyiwa hivyo na vyombo vya habari.
Aidha ,Mbunge wa viti maalum, Margareth Sitta anasema mpaka sasa Tanzania imeshindwa kurudisha shuleni wanafunzi wanaopata mimba ili waendelee na masomo pindi wanapojifungua.
"Tunapoteza wasichana wenye uwezo mkubwa, Nchini Kenya Mwanafunzi
anapojifungua anaruhusiwa kuendelea na masomo hapa Tanzania kuna nini?" anasema
Alitaka katiba iwe na kipengele cha kurudisha tena kwenye masomo
wanafunzi wanaopata ujauzito.
"Tuongeze kipengele hicho kwenye katiba hiii ili wanafunzii wanaopata
mimba waendelee na masomo.
Victoria Lihiru kutoka Ulingo anasema mchakato wa katiba haukusahau wanawake kutokana na kujitokeza kwa masuala mengi ya kijinsia.
Anasema rasimu ya pili imeweka wazi kuwa wanawake wote ni sawa.
"Kwenye tunu za taifa, amani haijatajwa ,usawa wa kijinsia haujatajwa ni suala la kupigia kelele ili vitu hivyo virudi" anasema
Anabainisha kuwa haki za wanawake zipo lakini hakuna tume ya kusimamia utekelezaji wake kwani katiba ni kitu kimoja na utekelezaji ni kitu kingine.
Pia haki za wanawake wenye ulemavu pia zimekosekana kwenye
rasimu ya pili ambayo pia haijasema haijasema nani ni mtoto kama ni miaka 18 au 21 katiba ni lazima iainishe mtoto ni nani.
"Hata vyama vya siasa havijabanwa kuzingatia masuala ya kjinsia pia
katika suala la kufanya maamuzi katiba imebaki kimya.Katika nchi
nyingine kuna bajeti katika masuala ya kijinsia yamekuwa yakitengewa bajeti na hivyo kurahisisha utekelezaji wa vipaumbele mbalimbali.
Aidha ,Mbunge wa viti maalum, Margareth Sitta anasema mpaka sasa Tanzania imeshindwa kurudisha shuleni wanafunzi wanaopata mimba ili waendelee na masomo pindi wanapojifungua.
"Tunapoteza wasichana wenye uwezo mkubwa, Nchini Kenya Mwanafunzi
anapojifungua anaruhusiwa kuendelea na masomo hapa Tanzania kuna nini?" anasema
Alitaka katiba iwe na kipengele cha kurudisha tena kwenye masomo
wanafunzi wanaopata ujauzito.
"Tuongeze kipengele hicho kwenye katiba hiii ili wanafunzii wanaopata
mimba waendelee na masomo.
Victoria Lihiru kutoka Ulingo anasema mchakato wa katiba haukusahau wanawake kutokana na kujitokeza kwa masuala mengi ya kijinsia.
Anasema rasimu ya pili imeweka wazi kuwa wanawake wote ni sawa.
"Kwenye tunu za taifa, amani haijatajwa ,usawa wa kijinsia haujatajwa ni suala la kupigia kelele ili vitu hivyo virudi" anasema
Anabainisha kuwa haki za wanawake zipo lakini hakuna tume ya kusimamia utekelezaji wake kwani katiba ni kitu kimoja na utekelezaji ni kitu kingine.
Pia haki za wanawake wenye ulemavu pia zimekosekana kwenye
rasimu ya pili ambayo pia haijasema haijasema nani ni mtoto kama ni miaka 18 au 21 katiba ni lazima iainishe mtoto ni nani.
"Hata vyama vya siasa havijabanwa kuzingatia masuala ya kjinsia pia
katika suala la kufanya maamuzi katiba imebaki kimya.Katika nchi
nyingine kuna bajeti katika masuala ya kijinsia yamekuwa yakitengewa bajeti na hivyo kurahisisha utekelezaji wa vipaumbele mbalimbali.
Aidha Mjumbe wa Bunge la katiba, Dk.Ave Maria
Semakafu anataka kuwe na tume ya kufuatilia masuala ya usawa wa kijinsia ambapo
Stella Jairos kutoka Sauti ya Wanawake wenye ulemavu Tanzania anasema walemavu
ni kundi pekee la unyonge ambalo huwezi kukwepa ukweli uliopo.
Pia anasema elimu
ni chanzo cha maarifa yote vilevile ni chanzo cha kila jambo wanawake
wenye ulemavu wafikiriwe kupewa nafasi za bure katika shule za msingi na
sekondari ili kuongeza idadi ya wanawake wanaopata elimu ambayo itawasaidia
katika maisha yao.
Vilevile anataka walemavu wathaminiwe katika suala
la usalama wa uzazi.
Pamoja na hayo hata katika masuala ya kodi yaangaliwe
kwani walemavu wasioona wamekuwa
wakiingia gharama mara mbili kutokana na kulipa watu wanaowaangoza
wakati kiwango cha malipo wanayofanyia kazi yakikatwa kodi na kupungua hali
inayofanya maisha kwao kuwa magumu.
Jairos anasema katika rasimu ya pili kulikuwa hakuna
makala za kutosha .
“Shirika la Oxfam lilifadhili nakala 50 nchi nzima
watu wengi wenye ulemavu rasimu ya pili hawaijui” anasema
Mbunge wa Kasulu Vijijini, kupitia Chama cha
NCCR-Mageuzi ,Agripina Buyogera anasema
sasa wanawake wamebadilika na kuwa na mshikamano sana.
Anasema alisimama na kugombea Ubunge kupitia jimbo
na alifanikiwa kuchaguliwa anaamini kama wakiingia 50/50 wanawake wanaweza.
Pia Mbunge huyo anasema sasa anasoma elimu ya
sekondarii ili aweze kupata cheti cha kidato cha nne kwani wakati akichaguliwa
kuwa Mbunge alikuwa na elimu ya darasa la saba na anajiendeleza ili aweze kuwa
na sifa za kugombea nafasi hiyo tena.
“Kutokana na umaskini sikubahatika kupata elimu
nikachaguliwa kuwa Mbunge nikiwa na elimu ya darasa la saba na sasa
najiendeleza, wanawake wanaweza” anasema
Anasema vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia na
udhalilishaji vimekuwa vikitokea mara kwa mara kuna wakati wanaona wanawake
wananyanyaswa na kubughudhiwa wajitahidi na kujenga ushujaa wa kujiamini.
![]() |
| Mwanasiasa Mkongwe Nchini, Anna Abdalah |
Subscribe to:
Comments (Atom)


