Friday, April 18, 2014

Polisi dodoma wajipanga kudhibiti uhalifu sikukuu ya Pasaka




JESHI la Polisi Mkoani Dodoma, limesema limejipanga kuimarisha ulinzi
maeneo yote ya Mkoa wa Dodoma katika kipindi chote cha sikukuu ya
pasaka.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Kamishna Msaidizi wa Polisi (SACP),
David Misime alisema katika kipindi cha pasaka Jeshi la polisi
limejipanga kuimarisha ulinzi maeneo yote ya mkoa wa Dodoma na
watafanya doria za miguu, pikipiki, magari na pia kutumia mbwa na
farasi.
Alisema kutokana na suala la ulinzi na usalama ni la kila mtu na wadau
mbalimbali na watashirikiana na vyombo vingine vya dola, manispaa
kampuni za ulinzi binafsi, viongozi wa serikali za mitaa na vikundi
vya ulinzi shirikishi.
“Tunachoomba ni kila mtu atambue ulinzi ni jukumu la kila moja na
unaanzia katika ngazi ya familia tunaomba waendelee kushirikiana na
Jeshi la polisi kwa kutupatia taarifa za wahalifu na uhalifu” alisema
 Alitaka kila  mtu azingatie sheria za usalama barabarani ili kuzuia
ajali,kuepuka ulevi wa kupindukia na sehemu za starehe wazingatie
sherehe.

No comments:

Post a Comment