Friday, December 6, 2013

Daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake akemea ukeketaji

DAKTARI bingwa wa magonjwa ya kinamama katika hospitali ya Mkoa wa Dodoma Dk Januarius Hinju amesema kinamama wajawazito 4,130 kati ya 20,361 waliojifungua katika hospitali ya Mkoa wa Dodoma katika kipindi cha mwaka 2011 na 2012 walikuwa wamekeketwa. Kauli hiyo ameitoa wakati wa mdahalo wa maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia kanda ya kati. Dk.Hinju alisema kwa mwaka 2011 jumla ya akinamama wajawazito 10,477 waliojifungua katika hospitali ya mkoa ambapo katiyao 2392 sawa na asilimia 23 walikuwa wamekeketwa ikiwa ni sawa na asilimia 56. Amesema kutokana na kukeketwa walikuwa na tatizo la kutokwa na damu nyingi hali iliyosababisha kuhatarisha kupoteza maisha. Aidha mwaka 2012 jumla ya kinamama wajawazito 9914 walijifungua ambapo kati yao 1748 walikuwa wamekeketwa wakiwa sawa na asilimia 62. Dk Hinju amesema ipo haja ya ya kufanyika utafiti wa kina ili kubaini tatizo la ukeketaji katika mkoa wa Dodoma limepungua au la kutokana na vitendo vya ukeketaji kuhatarisha maisha ya wanawake wengi wakati wa kujifungua. Amesema takwimu hizo ni za waliojifungulia katika hospitali ya mkoa pekee hali inayoonesha kuna uwezekano kuwa tatizo la ukeketaji badili linaendelea katika jamii. Daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake katika hospitali ya Mkoa wa Dodoma Januarius Hinju akizungumza wakati wa mdahalo wa siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia kanda ya kati.Mdahalo huo uliandaliwa na Mtandao wa Kupambana na Ukatili wa Kijinsia (MKUKI) unaoratibiwa na Shirika Lisilokuwa la Kiserikali la AFNET kwa kushirikiana na Shirika la WILFAF

No comments:

Post a Comment