Monday, December 23, 2013

Chama cha Waandishi Dodoma chakabidhiwa kompyuta tatu


KAMPUNI ya simu  ya Vodacom imekabidhi kompyuta tatu na mtambo wa kuunganisha kompyuta kwa Chama cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Dodoma (CPC)  vyote vikiwa na thamani ya Sh. Milioni 5.3
Mwakilishi wa kampuni hiyo, Salum Mzee amesema  kompyuta hizo zimetolewa ili kutimiza ahadi waliyoitoa na kutaka vifaa hivyo kutumika kwa ajili ya kusaidia kazi za uandishi wa habari Mkoani Dodoma
Amesema Vodacom  inatambua mchango wa waandishi wa habari kwa kutoa taarifa ambazo zimekuwa zikifikia jamii ambao ndiyo walengwa.

Mwakilishi huyo wa Vodacom amesema mwaka jana walipitisha mpango maalum wa kusaidia vyama vya waandishi wa habari ambapo Sh. Milioni 40 zilitengwa na hadi  sasa mikoa iliyofaidika ni pamoja na Tanga, Kagera, Iringa na Dodoma
Pia ameitaka CPC kuhakikisha vifaa hivyo vinatumika  kwa shughuli iliyokusudiwa ya kuanzia mradi wa internet.
Mgeni rasmi katika makabidhiano hayo Mkuu wa Wilaya ya Chamwino, Fatma Ally alitaka vifaa hivyo vitunzwe vizuri ili viweze kutumika kwa muda mrefu.


Mwakilishi wa Kampuni ya simu ya Vodacom, Salum Mzee akizungumza wakati wa kukabidhi kpmpyuta tatu kwa Chama cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Dodoma (CPC)

MKUU wa Wilaya ya Chamwino,Fatma Ally (kushoto) akimkabidhi kompyuta Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa habari Mkoa wa Dodoma Joyce Kasiki (kulia), katikati anayeshuhudia ni mwakilishi wa Kampuni ya simu ya Vodacom , Salum Mzee

No comments:

Post a Comment