Thursday, December 19, 2013

Watoto wasaidiwe kutohatarisha afya zao

Watoto Kijiji cha Mkakatika Wilaya ya bahi wakifurahia kuoga kwenye dimwi la maji ambayo si salama kufuatia mvua kuanza kunyesha kwenye wilaya hiyo
KUTOKANA na mvua kuanza kunyesha katika maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Dododoma, Wazazi wametakiwa kuwa makini na watoto wao ambao wengi wao wamekuwa wakipenda kuogolea katika madimbwi ya maji ikiwemo maji machafu.
 Kunyesha kwa mvua kumeleta shangwe kwa wakazi wengi wakiwemo watoto hali inayopelekea kuona hiyo ni fursa nzuri kwao kufurahia maji.
 Mkazi wa Bahi Mkoani Dodoma Pendo Alfonce alisema ni vizuri wazai wakawa makini kwa kuwazuia watoto wao kwenda kuoga kwani mvua zinazonyesha ni chache na maji yanayokjaa kwenye madimbwi pia ng'ombe wamekuwa wakitumia kunywa maji.
Watoto wa Kijiji cha Mkakatika Wilaya ya Bahi Mkoani Dodoma wakioga kwente dimbwi la maji machafu.
 Alisema kumekuwa na tabia ya watoto kwenda kuoga kwenye madimbwi kitui ambacho ni hatari kwa afya zao kwani wana hatari kubwa ya kuambukizwa magonjwa mbalimbali ikiwemo kichocho.

No comments:

Post a Comment