![]() |
| Mkazi
wa Dodoma, akichagua miti ya matunda kutoka kwa muuzaji kama alivyokuwa jana na kamera yetu |
Mwandishi wetu alishuhudia baadhi ya wauzaji wa miche ya miti mbalimbali ikiwemo ya kivuli, matunda na maua.
Mmoja wa wafanyabiashara hao Ayub Chitete alisema amekuwa akiuza mti moja wa matunda ana ya mchungwa kwa Sh. 2,000 na mche wa muembe kwa Sh. 3,000
Alisema miche ya maua na ile ya kivuli huuzwa kwa bei ya maelewano na mteja.
Alisema biashara hiyo imekuwa na changamoto nyingi ikiwemo wateja kuomba kupunguziwa bei licha ya kuwa kutunza miche hiyo kumekuwa ni harama kubwa.
Hata hivyo, baadhi ya wakazi wa Dodoma wakiongea na mwandishi walisema ni muhimu kama wananchi watapata hamasa ya kununua miche ya miti ili kuipanda kama sehemu ya kuboresha mazingira.


No comments:
Post a Comment