Tuesday, November 12, 2013

Mulugo ashinda shindano la kucheza muziki

NAIBU Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philip Mulugo (Wa tatu kutoka kulia) akicheza muziki na wahitimu wa Chuo cha Mafunzo ya Ufundi (VETA) Dodoma mwishoni mwa wiki ambapo aliibuka mshindi

NAIBU Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi,Philip Mulugo juzi aliibuka mshindi katika shindano la kucheza muziki  wa kwaito wakati wa mahafali ya 30 ya Chuo cha Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) Dodoma
Mulugo alikuwa akishindana pamoja na wahitimu wa fani mbalimbali ambao baadaye aliwatunikia vyeti.
Mshindi wa shindano hilo alipatikana kutokana na maoni ya wanafunzi na wazazi ambao walikuwepo katika mahafali hayo.
Akimtangaza mshindi huyo Mkuu wa Chuo cha VETA Dodoma, Ramadhani Mataka alisema Naibu Waziri Mulugo atapata zawadi ya kuchongewa kitanda cha futi sita kwa sita ambacho kitakuwa ni ukumbusho mzuri kwake.
“Tutakuchongea kitanda cha futi sita kwa sita ambacho nadhani utakipeleka jimboni mwako kiwe kwa ajili ya kupumzikia” alisema Mataka
Jumla ya wahitimu 122 walitunukiwa vyeti katika fani mbalimbali, ikiwemo, ujenzi, umeme na udereva
Licha ya mahafali hayo kupambwa na burudani mbalimbali pia kulikuwa na onesho la mavazi yaliyoandaliwa na wanafunzi wa Chuo hicho.

No comments:

Post a Comment