MKUU wa Wilaya Mpya ya Chemba Mkoani
Dodoma, Francis Isaack amesema tayari Wilaya hiyo imeanza mikakati ya kuunda
vikundi vya vijana kwa lengo la kuwawezesha kushiriki kikamilifu katika
shughuli za kilimo.
Pia Mkuu huyo wa Wilaya alisema ujenzi
wa nyumba na ofisi ya Mkuu wa Wilaya hiyo inatarajia kukamilika Julai mwakani.
Alisema sasa wakandarasi wa ujenzi
huo wanaendelea na hatua mbalimbali za
ujenzi na kuanzia Julai mwakani shughuli nyingi za kiserikali zitahamishiwa Wilayani humo.Aidha alibainisha kuwa Hospitali ya Wilaya ya Wilaya hiyo itajengwa kwa nguvu za wananchi kwa kushirikiana na Serikali ambapo wananchi watachangia tofali,kokoto na mchanga.
Chemba ni Wilaya mpya katika Mkoa wa Dodoma iliyoanzishwa mwaka 2012 baada ya kugawanywa kwa Wilaya ya Kondoa.
No comments:
Post a Comment