BAADHI ya wakazi wa Kijiji
cha Chiboli, wilaya ya Chamwino Mkoani hapa hawana mahali pa kuishi baada ya
nyumba zao kuezuliwa na upepo mkali ulioambatana na mvua kubwa.
Akizungumza Kijijini hapo, Diwani wa Kata ya Chiboli,
William Teyu alisema mvua hiyo ilinyesha juzi kuanzia saa 11 jioni na kudumu zaidi ya saa moja.
Alisema madhara
yaliyosababishwa na mvua hiyo ni pamoja na kuezuliwa kwa nyumba 11 na uharibifu
wa vitu mbalimbali vikiwemo vyakula, umeme wa jua ,radio na simu.
Diwani huyo alisema miongoni
mwa nyumba zilizoezuliwa nane kati ya nyumba hizo ni za wananchi wa kawaida,mbili nyumba za
walimu na moja ya kwake mwenyewe (Diwani)
Alisema kutokana na janga
hilo wananchi hao hivi sasa wanaishi kwa majrani huku wengine wakiishi kwenye vyumba
walivyokuwa wakivitumia kama majiko ya kupikia na stoo za kuhifadhia chakula.
Kwa upande wake, Mkurugenzi
wa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino, Adrian Jungu ameahidi kupeleka wataalamu
kwa ajili ya kufanya tathimini kuhusu madhara yaliyosababisha na mvua hiyo.
Pamoja na hayo alisema
wataangalia namna ya kuwasaidia wananchi waliopata madhara hayo.
No comments:
Post a Comment