Wednesday, November 6, 2013

TRA WAPANIA MAKUBWA


MENEJA wa Mamlaka ya Mapato Tanzania, (TRA) Mkoa wa Dodoma , Thadey Kaliza amesema wanakusudia kukusanya kiasi cha Sh. Bilioni 37 katika mwaka wa fedha wa  Julai 2013 hadi Juni 2014 .

Alisema hayo juzi katika mkutano wake na waandishi wa habari juu ya Wiki ya Mlipa Kodi na kuwataka wafanyabiashara kuona fahari kulioa kodi kwa ajili ya maendeleo ya taifa.

Alisema katika mwaka huu wa fedha serikali imewapangia  mkoa huo kukusanya kiasi cha Sh. Bilioni 37 na kuongeza kuwa hiyo ni changamoto kubwa kwao.

Kaliza alisema mwaka uliopita  mkoa wa Dodoma ulipangiwa kukusanya  jumla ya Sh. bilioni 24.5 sawa na asilimia 93.5 huku lengo likiwa ni kukusanya  bilioni 26.

Aidha alisema ongezeo hilo la mwaka huu, TRA kutakiwa kukusanya Sh. bilioni 37 ni sawa na asilimia 10.

Alisema  Watanzana wengi hawajisikii fahali kulipa kodi kwa faida ya maendeleo ya Taifa na badala yake wanaona ufahali kukwepa kulipa kodi.
Aliwataka Watanzania kujenga utamaduni wa kudai risiti pindi wanaponunua bidhaa mbalimbali ili kusaidia Nchi kukusanya mapato.
Alisema taaluma ya kodi ina changamoto nyingi lakini cha msingi ni kuangalia jinsi gani walipa kodi wanavyoangalia suala hilo na lina faida gani kwao.
Alisema ni muhimu kwa wafanyabiashara kuwa na mashine unakuwa na uhakika na kile unachokipata katika biashara.

No comments:

Post a Comment